Huduma ya Assaph ambayo makao yake makuu ni hapa Dar es
Salaam itafungua tawi lake jingine huko Mkoani Dodoma, Kanisa hilo
litafunguliwa eneo la kisasa ambalo ni makazi mapya kwa wakazi wa mkoa huo,
kama ilivyo kauli Mbiu ya Assaph ni Uponyaji wa Yesu kwa Mataifa yote sasa
uponyaji huo utawafikia wakazi wa mkoa wa Dodoma na vitongoji vyake. Mchungaji
Israel John ambaye ndiye msimamiaji wa kanisa hilo amesema kazi imesha anza na
watu wameanza kupokea miujiza yao. Jumapili iliyopita ibada ya kwanza
imefanyika huko Dodoma, watu wote waishio Dodoma mjini wanakaribishwa kukutana
na nguvu za Mungu zitakazowafanya kuweza kufunguliwa kutoka katika vifungo
vyao.
 |
| Apostle Assaph Benja na mkwewe wabeba maono wa Assaph Ministries |
Akiongea kwa njia ya simu alisema kuna mama mmoja ambaye
alikuwa anasumbuliwa na uvimbe kwa muda mrefu ameombewa na kutapika finyango za
nyama ambazo alilishwa mwaka 90, na kupona kabisa, mama huyo alisema Alisha zunguka
kwenye hospital nyingi na alionekana na huo uvimbe ila akipelekwa chumba cha
upasuaji uvimbe unapotea lakini kwa jina la Yesu sasa amekuwa mzima kabisa.
 |
| Pastor Israel anayesimamia kanisa la Dodoma |
Unaweza kuwasiliana na watumishi hawa kwa no zifuatazo Apostle Ben 0782499991 na watu wa Dodoma Pastor Israel 0786836591