assaph

assaph

Sunday, 25 May 2014

PICHA ZA IBADA ASSAPH MINISTRIES INTERNATIONAL

Picha za ibada huduma ya Assaph chini ya mtume na nabii Assaph ben

IBADA YA KUBARIKI WATOTO

Ibada ya Leo pamoja mambo mengine yaliyokuwepo ni kuwaweka wakfu watoto. Mtumishi was Mungu mtume na nabii Assaph Ben ndiye aliyeongoza ibada hiyo.

IBADA YA KUBARIKI WATOTO

Ibada ya Leo pamoja mambo mengine yaliyokuwepo ni kuwaweka wakfu watoto. Mtumishi was Mungu mtume na nabii Assaph Ben ndiye aliyeongoza ibada hiyo.

Tuesday, 13 May 2014

MAOMBI YA KULIOMBEA TAIFA LA TANZANIA

Tangu Mch Kiongozi wa kanisa la Assaph ministries International aonyweshwe maono ya vita itayo ipata Tanzania kama hakutakuwa na toba na maombi ya kuomba rehema, kanisa limeingia katika maombi ya kuombea nchi.

Akiongoza maombi hayo mama Mch alifundisha andiko kutoka katika kitabu cha 2nyakati 7:14 ikiwa watu wangu, walioitwa kwa jina langu, watajinyenyekesha , na kuomba na kuutafuta uso, na kuziacha njia zao mbaya; basi nitasikia toka mbinguni na kuwasamehe dhambi yao na kuiponya nchi yao. Vile alisema tunatakiwa kuwaombea viongozi wa nchi ili wasije ipeleka nchi katika majanga ila Mungu awape hekima na busara katika kuongoza nchi.

Alisoma andiko lingine 2timoth 2:1-2 basi kabla ya mambo yote nataka dua, na sala na maombezi na shukrani zifanyike kwaajili ya watu wote. Kwa ajili ya wafalme na wote wenye mamlaka tuiishi maisha ya utulivu na amani katika utauwa wote na ustahivu.

Baadae maombi yalifanyika tunahamasisha kila atakae soma habari hii aingie kwenye maombi ya kuombea nchi na washirikishe na wengine. Amen

Sunday, 11 May 2014

Mahubiri yaliyo recodiwa live kutoka ibadani, Mwl Rachel wa Assaph Ministries



 Sikiliza mahubiri ya leo Jumapili ya Tar 11/05/2014

Mwl Rachel wa Assaph Ministries

PATA KIONJO CHA WIMBO MPYA WA SAMMY~SHITUKA

SAMMY~SHITUKA

KAMA UNA MAONI YOYOTE NIANDIKIE HAPO CHINI AU TUMA UJUMBE KWENYE NO +255 715 033 671, +255 767 033 671 AU FB Martin Malecela follow me in Twetter martmalecela au tembelea page yetu na ulike martmalecela.blogspot.com

Saturday, 10 May 2014

MTUMISHI REV BEN AONYESHWA MAONO YA VITA KATIKA NCHI YA TANZANA MAOMBI YAHITAJIKA KUNISURU

Mchungaji Kiongozi wa huduma ya Assaph Ministries International Rev Ben, hivi karibuni alionyeshwa katika maono nchi ya Tanzania ikiwa katika vita kubwa. Mtumishi amesema hii ni Mara ya tatu sasa anaonyeshwa na hii imekuwa ni kubwa hata kumfanya baada ya kutoka kwenye maono hayo moyo kumwenda mbio. Alieleza aliona jinsi watu watakavyopata shida katika kukbia hasa watoto akina mama na wazee.


Ikumbukwe miaka ya hivi karibuni kumekuwa na mivutano mbali mbali ya kisiasa na mihemuko ya wanajamii katika sehemu mbalimbali na kusababisha hata baadhi ya watu kupoteza maisha bila hatia lakini pia kumeongezeka maasi yanayotokana na kuporomoka kwa maadili na mabaliko ya kijamii yatokanayo na utandawazi. 

Lakini kumekuwa na mihemuko ya kidini sehemu ambayo imesababisha vurugu za hapa na pale na hata watu kumwagiwa tindi Kali na utumiwaji wa siraha za moto kama risasi na mabomu. Katika maelezo Yake amesema kuna msukumo wa chini kwa chini kutoka nchi nyingine kwa kutaka kuharibu tu amani iliyopo Tanzania. Wanajiuliza kwanini Tanzania iwe na amani tuuu wanaweza hata kutumia pesa kuwatumia baadhi ya watanzania kutuvuruga, aliuliza kama Tanzania kutatokea vita tutakimbilia wapi? Maana majirani wote wanaotuzunguka si swali. Alimaliza kwa kusema anatamani watanzania wapate ujumbe huu ili kwa pamoja tuungane kuombea amani nchi yetu ya Tanzania.

 Mungu anasema katika kitabu cha 2nyakati 7:14  Ikiwa watu wangu, walioitwa kwa jina langu, watajinyenyekesha, na kuomba, na kunitafuta uso, na kuziacha njia zao mbaya; basi, nitasikia toka mbinguni, na kuiponya nchi yao.  hivyo hata mtu mmoja akimaanisha basi Mungu yuko kusikia na kughaili hivyo watanzania tunahamasisha kuiombea inchi Yetu ili Mungu atunusuru na vita.

Ikumbukwe huko nyuma kulikuwa na huduma ya Tanzania itubu ambayo ilihamasisha watanzania kutubu ili tusipatwe na majanga ni wakati wa kumrudia Muumba wetu ili aiponye inchi yetu.

Monday, 5 May 2014

IBADA YA JUMAPILI TAR 04/05/2014 KATIKA PICHA, ONJENI MUONE BWANA YU MWEMAHAPA

Katika Ibada ya Jana tulimwona Mungu akiponya na kuokoa, watu wanaendelea kupokeamiujiza yao na wengine wanampokea Yesu kuwa Bwana wa Maisha yao. Wiki hii kuna mwanamziki mashuhuli ameokoka yeye Anaitwa Dede ni mpiga ala za muziki na ni mtaalamu wa Studio. Nilifanya nae maongezi na kunidokeza kuwa yeye ndiye aliyepiga gita kwenye album ya marehemu Remmy Ongala ile ya gospel na kwa sasa anapigia kwenye bendi maarufu sana ya king Kiki hapa Dar. Sifa na utukufu kwa Bwana. vile vile alikuwapo Rungu la Yesu mwimbaji wa hip hop hapa TZ ambaye yeye yuko na kauli mbiu Yesu Okoa Mitaa YOM tulimwona Bwana akimtumia.
Rungu la Yesu alitutembelea na kuimba na ujumbe wake wa YOM

Huyu ni Dede mpigaji ala maarufu hapa Tz ameamua kuokoka
watoto wa Yesu
Mtumishi Rachael akiombea wahitaji
uweponi mwa Bwana
Papa Ever akimshukuru Mungu kwa jinsi anavyompigania na kumtetea kila itwapo leo
Maombezi
HAPA MTUMISHI WA MUNGU ALIKUWA ANAFUNDISHA SOMO KUTOKA KITABU CHA AYUBU 38 :12-13
Rungu la Yesu akiimba
Maombezi
mama huyu alishuhudia baada ya kuponywa alikuwa amepooza mwili mzima baada ya maombezi Mungu amemponya na sasa yuko mzima kabisa